G&P

Grace & Patrick

Wedding Songbook

Songs

No matching song found.
Wedding Songs#1

TUFURAHI SOTE KATIKA BWANA

{ Tufurahi sote katika Bwana,

Tunapoadhimisha siku kuu

Kwa heshima ya bikira Maria } *2

Malaika wanafurahia kupalizwa kwake mbinguni

Na wanamsifu mwana wa Mungu aleluya

Bwana amewafunulia mataifa wokovu wake

Ameidhihirisha haki yake aleluya

Atukuzwe Baba na mwana na Roho Mtakatifu

Kama mwanzo sasa na siku zote

Wedding Songs#2

TUFURAHI

Tufurahi - Mungu wetu atupenda wanae wote

Tufurahi - Mungu wetu atupenda wanae

Watu wote - wanameremeta tazama

Wamevaa - mavazi mazuri oneni

Nyuso zao - tabasamu shangwe nderemo na vifijo *2

Ndugu yangu -

Tupendane -Tuimbe wote -

Tufurahi -

Mungu wetu -

Atuinua -

Atupenda -

Atuinua -

Pendo gani -

Ametupa -

Wedding Songs#3

NJOONI TUMFANYIE SHANGWE MUNGU WETU

Njooni tumfanyie shangwe Mungu wetu

Njooni tumfanyie shangwe Mungu wetu

Jiungeni wote tuimbe pamoja

Njooni tumfanyie shangwe Mungu wetu

Kwa miondoko ya raha na kucheza

Njooni tumfanyie shangwe Mungu wetu

Kwa ngoma safi tamu na za midundiko

Njooni tumfanyie shangwe Mungu wetu

(Tumpigie) makofi makofi makofi

(Tumpigie) makofi makofi makofi

(Tumpigie) makofi makofi makofi

makofi

Bwana ametenda wema wa ajabu -

Machozi ameyageuza vicheko -

Tumwimbie leo tumsifu yeye -

Tukipigapiga vifua kwa maringo -

Tumpungieni mikono kwa madaha -

Ajue kwamba leo tumefurahi -

Na shingo zinesenese kwa midundo -

Mwili uyumbeyumbe kushoto kulia -

Watoto nao wabebwe juu juu -

Wajue kwamba Mungu anawapenda -

Umati wote urukeruke juu -

Tusisite Mungu yu katikati yetu -

Misa Subukia#4

BWANA BWANA UTUHURUMIE

Bwana, Bwana, Bwana utuhurumie *2

Kristu utuhurumie, Kristu utuhurumie *2

Bwana, Bwana, Bwana utuhurumie *2

Misa Subukia#5

UTUKUFU JUU KWA MUNGU (SUBUKIA)

{ Utukufu juu kwa Mungu, na amani duniani,

kwao watu wenye mapenzi,watu Aliowarithia } *2

Tunakusifu tunakuheshimu, twakuabudu tunakutukuza, Twakushukuru kwa ajili yako, ya utukufu wako mkuu.

Ee Mungu baba ndiwe mfalme, Mfalme wa Mbinguni baba mwenyezi.

Ee Yesu Kristu mwana wa pekee, mwanakondoo mwana wa Baba.

Uondoaye dhambi za watu tuhurumie tusikilize, Tuhurumie mwenye rehema maombi yetu uyapokee.

Uketiye kuume kwake, Mungu baba tuhurumie. Kwa kuwa ndiwe pekee yako, Pekee yako Mtakatifu.

Pamoja naye roho Mtakatifu, katika utukufu wake. Anayeishi na kutawala, milele yote Amina.

Misa Subukia#6

NASIKIA SAUTI NZURI

Nasikia sauti nzuri kama ya malaika

Ni sauti toka mbinguni, sauti ya Mungu

Aniita mimi niende nikamtumikie

Anitume shambani mwake nikavune yote

Umeniita, nimeitika wito, nakuja kwako leo,

najongea mbele zako Bwana nipokee mimi,

niko tayari, nimeyaacha yote,

najikabidhi kwako,

unitume popote nami nitakwenda haraka

Ninaenda mimi naenda, ninaenda mwenyewe, ninaenda mbele za Bwana,

sitarudi nyuma. Ndugu zangu na marafiki, mniache niende,nikafanye kazi ya Bwana, nitakapotumwa .

Nilitazama moyo wako, moyo wako mwanangu, hata kabla hujazaliwa, nilikutambua,

nilikuteua mapema kati ya ndugu zako, uwekuhani wangu mimi, kuhani mkuu.

Shamba lake Bwana ni kubwa na

mavuno ni mengi,

wavunaji ndio wachache nitakwenda mimi,

nakuomba sana ee Bwana,

nipeleke shambani,

nikavune mavuno yote yaliyo tayari.

Uwe nami siku kwa siku, Bwana usiniache

unikinge na majaribu nilinde daima

nipeleke habari njema, ulimwenguni mwote,

watu wote wakutambue, wakugeukie.

Misa Subukia#7

NTHEMBO TENE NISYAUMAWA

Nthembo tene nisyaumaw'a - ni etikili ivinda ya tene

Syaumaw'a na kuvivywa - nthembo kwa Ngai Asa

Tumuthembee - Ngai tumuthembee *2

Na makwasi - Ngai tumuthembee

Na malenge - Ngai tumuthembee

Tumuthembee - Ngai tumuthembee

Avalamu niwaumisye nthembo ya mwana wake

Amuthembee Ngai Asa ni kana amuathime

Ithyi andu tumuthembee NgaiAsa atutavisye

Tumuthembee ithyi andu nikana atuathime

Syindu ila twinasyo mbemba na mboso syonthe ni syake

Mbui na ng'ombe nduma na maiu, syonthe tumuthembee

Tumuthembee ithyi andu - Ngai Asa atutavisye

Tumuthembee Ngai Asa - Nikana atuathime

Misa Subukia#8

WE ASA OSA

{ We Asa osa nthembo yaitu,

We Asa osa na uituathima } *2

{ Na Mukate wumite nganuni ya nthi

We Asa osa na uituathima } *2

Na ndivai yumite nzavivuni . . .

Na mbesa syumite mivukoni . . .

Na ngetha yumite miundani . . .

Na malondu maumite ndithyani yitu . . .

Misa Subukia#9

MTAKATIFU (SUBUKIA)

Mtakatifu Mtakatifu Mtakatifu Mungu wa majeshi

Mbingu na dunia zimejaa, zimejaa utukufu wako.

Hosanna hosanna hosanna hosanna juu mbinguni

Mbarikiwa anayekuja anayekuja kwa Jina la Bwana

Misa Subukia#10

MWANAKONDOO

No lyrics were included under this heading in the source document.

Misa Subukia#11

NITAIJONGEA ALTARI YA BWANA

Nitaijongea altari ya Bwana (Yesu)

Nami nishiriki karamu yake,

yenye upendo na mapatano,

nijipatie amani moyoni mwangu.×2

1. Unilishe mwili wako ,we Bwana mwokozi wangu-

nijipatie amani moyoni mwangu

2. Uninyweshe damu yako,ee Yesu mkombozi wangu

3. Uwe nami siku zote,katika maisha yangu -.......

4. Usiniache Bwana wangu,wewe ni uzima wangu

5. Ukae nda-a-ni yangu unipe wokovu wako.....

6. Unilinde Bwana wangu,mimi mjakazi wako

Misa Subukia#12

TARORA IRATHIMO

Tarora irathimo wone, wone, wone

Uria Ngai ekite, wone

Ngai ari hamwe na andu ake

Tarora irathimo wone, wone, wone

Uria Ngai ekite, wone

Ngai ari hamwe na andu ake

Kuma twaigwa mugambo wa Mwathani

Ngai ari hamwe na andu ake

Waingira ngoroini riu no gwathika

Ngai ari hamwe na andu ake

Irathimo nacio ikaura ta mbura

Ngai ari hamwe na andu ake

Micii itu Ngai ni arathimite

Ngai ari hamwe na andu ake

Wendo na gikeno ituraga na ithui

Ngai ari hamwe na andu ake

Ciana ciitu nacio niciathikaga

Ngai ari hamwe na andu ake

Mawira ma moko niarathimite

Ngai ari hamwe na andu ake

Makubi maitu no kuihuririra

Ngai ari hamwe na andu ake

Tuhune ngoro na miiri itu

Ngai ari hamwe na andu ake

Kwaya itu Ngai niarathimite

Ngai ari hamwe na andu ake

Tuinagira Ngai twina gikeno

Ngai ari hamwe na andu ake

Kuirutira gwitu Ngai niarathimite

Ngai ari hamwe na andu ake

Misa Subukia#13

MOYO WANGU WAMTUKUZA BWANA

{(Moyo) Moyo wangu wamtukuza Bwana

(Roho) Roho yangu inafurahi }*2

Kwa kuwa amemwangalia, kwa huruma mtumishi wake

Hivyo tangu sasa watu wote, wataniita mwenye heri

Kwa sababu Mwenyezi Mungu, amenifanyia makuu

Jina lake ni takatifu,

Huruma yake ni kwa wote, wote wale wanaomcha

Kizazi hata na kizazi,

Huyatenda mambo makuu, kwa nguvu za mkono wake

Wenye kiburi hutawanywa,

Hushusha wote wenye vyeo, kutoka vitini vya enzi

Nao wale wanyenyekevu, wote hao huwainua

Huwashibisha wenye njaa, na matajiri huwaacha

Waende mikono mitupu,

Hulilinda taifa lake, teule la mtumishi wake

Akikumbuka huruma yake,

Kama alivyowaahidia, babu zetu kuwaahidia

Ibrahimu na mzao wake,

Atukuzwe Baba na Mwana, naye Roho Mtakatifu

Leo kesho hata milele, kwa shangwe milele amina.

Ndoa#14

I LOVE YOU

Siku tuliyoingoja mimi na wewe,

Kwa uwezo wake mungu leo imefika,

Popote uendapo tutakuwa pamoja

{Mungu ametuunganisha mimi nawe,

nasi wawili tena ni mwili mmoja,

wewe ni wangu kweli

na mimi ni wako njoo,

I love you mpenzi wangu

I need you siku zote I love you) *2

Kwa maombezi yake mama yetu maria,

Ahadi yetu sasa kweli imetimia,

Chaguo la moyo wangu mimi nakupenda,

Tulizo la moyo wangu njoo karibu yangu,

Nimekuchagua wewe wangu wa maisha,

Agizo la moyo wangu njo tujitulize,

Mpenzi wangu nakupenda nawe unipende,

Kwa penzi la raha na karaha tupendane.

Ndoa#15

HARUSI KIDEDEDEDE

{ Bwana harusi na bibi harusi, leo mmefunga ndoa ya maisha,

Kaeni kwa amani kidededede } * 2

Upendo wenu umedhihirika

Uyani kwenu bamba ishini tototo

Uzuri wenu hauna kifani

Uyani kwenu bamba ishini tototo

Na nyumba yenu imebarikiwa

Uyani kwenu bamba ishini tototo ooo

Jitulize mjisikie sukari, siku ya leo ni yenu,

Furahini, mmepambwa maua mnapendeza

Bwana arusi kwanza wachangamka, bibi arusi chachawa,

Chezacheza, penzi lenu leo limekamilika

Mapenzi yenu yote yatasitawi, hakika yatasitawi,

Yatamea, kama ule mwerezi wa Lebanoni

Baraka zake Mungu ziwashukie, kaeni pasipo shida,

Siku zote nyumba yenu iwe hekalu la Mungu.

Ndoa#16

PINGU ZA MAISHA

Pingu za maisha leo mmeshazifunga

Sasa ilobaki harusi yenu kuitunza *2

Muitunze harusi yenu - isije chafuka

Harusi yenu - isije chafuka

Muitunze na pete yenu - isije chafuka

Na pete yenu - isije chafuka

Muwatunze watoto wenu - wasije chafuka

Watoto wenu - wasije chafuka

Sasa ilobaki, harusi yenu kuitunza *2

Pete ni alama sote tumeshuhudia *2

Sasa ilobaki harusi yenu kuitunza *2

Ukifika huko dada kaa ukijua *2

Kaa ukijua dunia ina maneno

No matching song found.
Text